Tanzania: Nasha: Serikali kushirikiana na sekta binafsi kuboresha elimu

Tanzania / Mei 20, 2018 / Mwandishi: Wahariri wa Watumishi / Chanzo: Nijuze

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezipongeza shule za sekta binafsi kwa ulipaji mzuri wa kodi na kutambua umuhimu wake katika kuleta maendeleo ya Taifa.

Hayo yamezungumzwa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ole Nasha ameeleza kuwa kwa kutambua ushirikiano ulipo na sekta binafsi imekuwa ikiondoa changamoto zinazowakabili wamiliki wa shule hizo kama kuondoa kodi na tozo mbalimbali.

“Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kubora mazingira ya wao katika elimu, tutaendelea kuboresha zaidi ili wafanye kuwekeza kwa kiurahisi lakini vile vile naomba niseme kwamba sekta binafsi wamekuwa walipaji wazuri wa kodi na wanatambua umuhimu wa kulipa kodi katika maendeleo ya Taifa kwa hiyo na kwamba tupo pamoja katika kukabiliana nao kuhusiana na namba ya kuweza kuangalia namna ya kupunguza hizo kodi bado tunasisitiza kwamba ni vizuri tukaendelea kushirikiana ili kuhakikishia baadhi ya gharama ambazo ni mhimu ziweze kulipwa na wale ambao wanaweza kuchangia”

Aidha, serikali imedai bado inatambua vizuri kabisa umuhimu wa sekta binafsi katika utoaji wa elimu ili kuhakikisha mazingira rafiki katika utoaji wa elimu, serikali imejizatiti kufanya majadiliano na sekta binafsi kwa lengo la kuondoa changamoto zinazowakabili hadi sasa serikali imefanikiwa kuondoa kodi na tozo mbalimbali ambazo awali walikuwa wakitozwa wamiliki wa shule binafsi.

Chanzo cha Habari:

http://www.nijuze.co.tz/kitaifa/nasha-serikali-kushirikiana-na-sekta-binafsi-kuboresha-elimu/

Comparte este contenido:

Tanzania: Wazazi na Walezi wameiyomba serikali kuwachukulia hatua za kisheria walimu

Tanzania / Aprili 22, 2018 / Mwandishi: mik-dadi / Chanzo: Zanzibar 24

Baadhi ya Wazazi na Walezi wa Mkoa wa Kusini Unguja wameiomba serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwachukulia hatua za kisheria walimu wanaokataa kuwapokea wananfunzi wenye ulemavu katika skuli ili wanafunzi hao waweze kunufaika na elimu.

Wakizungumza na Zanzibar24  kwa maskitiko makubwa kwa niaba ya wananchi hao Mwenyetiti wa watu wenye Ulemavu Wilaya ya Kati Yunus Kassim na Mratibu wa wanawake na watoto Shehia ya kikungwi Bahati Issa wamesema kumejitokeza tabia kwa baadhi ya Walimu kuwakaa wanafunzi wenye ulemavu wakati wanapoenda kuandikishwa.

Wamesema kila mwananchi ana haki ya kupata haki zao za msingi hivyo wanashangazwa na baadhi ya walimu kuwakataa wanafunzi hao bila ya wananchi kujua sababu za msingi za kukataliwa kwa watoto wao.

Wamesema wakati umefika kwa maafisa Elimu kufatilia skuli ambazo zinaendelea na tabia hiyo ili walimu waweze kuchukuliwa hatua za kisheria na watoto waweze kunufaika na haki zao za kupata elimu katika nchi yao.

Aidha wametowa wito kwa Wizara ya Elimu na Mfunzo ya amali Zanzibar kuwapa mafunzo walimu ya kuwasomesha wanafunzi wenye mahitaji maalumu hususani wenye ulemavu wa kusikia katika skuli ili wanafunzi hao waweze kufahamu wanachosomesha wakiwa madarasani.

Kwa upande wake Afisa Elimu na Mafunzo ya amali Mkowa wa Kusini Unguja Abdallah Makame Makame amewaka Wazazi hao kuripoti katika Ofisi yake yanapotokeza matatizo hayo ili walimu waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Amesema mapka sasa hakuna kesi iliyoripotiwa lakini wazazi hao wanaendelea kulalamika mitaani jambo ambalo ni kinyume na sheria na wanasababisha watoto wao kutopata haki zao za misngi katika elimu.

Amesema azma ya serikali ni kuona kila mwananchi ananufaika na haki zake za msingi ikiwemo kupata matibabu na elimu hivyo si vyema kwa wazazi na walezi kuendekeza muhali katika kuwaripoti walimu wanaokiuka majukumu yao kwa wanafunzi.

Chanzo cha Habari:

Wazazi na Walezi wameiyomba serikali kuwachukulia hatua za kisheria walimu

Comparte este contenido:

Tanzania: SMZ yaahidi kuendelea kuimarisha Sekta ya elimu ya juu

Tanzania / Machi 25, 2018 / Mwandishi: Rasimu / Chanzo: Zanzibar24

Serikali ya mapinduzi zanzibar imesema itaendelea  najitihada zake za kuimarisha  sekta ya  elimu hususan  elimu ya vyuo vikuu kwa lengo la kukuza uchumi na maendeleo ya taifa .

Waziri wa biashara na viwanda  zanzibar mhe balozi Amina Salum Ali  ameyaeleza  hayo wakati  akizungumza  na wana funzi wa chuo  cha utawala wa umma tunguu katika  sherehe za siku ya serekali  ya wanafunzi  wa chuo hicho  (  zipaso day).

Amesema ili taifa liweze kukabilana vyema na kasi ya ukuaji wa uchumi  linahitaji kupata  wataalam waliobobea kupitia fani mbali mbali zikiwemo za kibiashara  hivyo serekali haitasita  kuongeza kasi ya uimarishaji wa sekta hiyo ili kuona kwamba wananchi wake na hasa vijana wanaingia  katika soko la  ajira  na kuweza kufikia malengo.

Hivyo balozi Amina amewataka vijana  na watumishi wa  umma  kuzichangamkia fursa  zilizopo ikiwa ni pamoja  na kujiunga  na vyuo  kujiongezea taluma  ili kuweza  kuleta mafanikio.

Aidha  ameutaka  uongozi wa  chuo  hicho kuendelea kutoa elimu bora  hasa kwa watumishi  wa umma ili watapotoka hapo waweze kulitumikia  vyema taifa  na kuleta maslahi kwa jamii.

Nao katika risala yao wanafunzi  hao wamesema licha ya mafanikio waliyoyapata  lakini bado wanakabiliwa na changamoto  mbali mbali zikiwemo  uhaba wa vitendeakazi,uhaba wa vifaa vya matibabu na dawa katika sehemu ya afya ,uchache wa vitabu ,na ukosefu wa uzio katika eneo la chuo.

Chanzo cha Habari:

SMZ yaahidi kuendelea kuimarisha Sekta ya elimu ya juu

Comparte este contenido:

Tanzania: wizara ya elimu imewataka walimu nchini watakiwa kujiendeleza kitaaluma

Tanzania / Februari 25, 2018Mwandishi: Chanzo: zanzibar24

Wizara ya  elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar imewataka walimu nchni kujiendeleza kitaaluma ili kutoa elimu inayoendana  na mahitaji ya wanafunzi  katika kuengeza ufaulu wa masomo yao.
 Akizungumza katika mkutano uliyowakutanisha wadau wa sekta ya elimu katika kujadili tathmini ya masomo kwa mwaka mzima, Kaimu waziri wa Wizara ya Elimu Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo amesema fani ya elimu imekuwa ikishushwa hadhi kutokana na baadhi ya walimu kushindwa kujiendeleza kitaaluma.
Amesema imefika wakati kwa walimu kujua umuhimu wa kazi zao katika kutoa elimu bora kwa wanafunzi ili waweze kunufaika na elimu inayotolewa katika skuli pamoja na kuengeza kasi ya kuzalisha wataalamu wa fani mbalimbali Nchi.
Aidha Kaimu kombo ametowa wito kwa Wazazi kuengeza kushirikiana na walimu katika kufatilia maendeleo ya wanafunzi ili kuwaengezea walimu ari ya kusomesha jambo ambalo litasaidia kurejesha hadhi na heshima ya walimu Nchini.
 Kwa upande wake Mwakilishi wa mtandao wa Elimu Zanzibar khamis Saidi ametowa wito kwa serikali kuwashirikisha wadau wa sekta ya elimu katika kuandaa bajeti ya sekta hiyo ili bajeti hiyo iweze kutumika kwa mahitaji yaliyokusudiwa .
Aidha amesema sekta ya elimu inahitaji mashirikiano mazuri baina ya serikali na wadau wa maendeleo ili kujua namna ya kuengeza ufaulu kwa wanafunzi.
 Nae mwakilishi kutoka Shirika la kuhudumia watoto nchini UNICEF Masoud Muhammed amesema wataendelea kuuunga mkono juhudi za serikali katika kutatua matatizo yanayo ikabilia sekta ya elimu.
Amesema mpaka sasa kuna matatizo mbalimbali ambayo yansababisha wananfunzi kutopata elimu ipasavyo ikiwemo wingi wa wananfunzi madarasani.
Amesea tatizo hilo pia la waingi wa wananfunzi maskulini linachangi baadhi ya wananfunzi kutoandikishwa skuli na wazeee wao jambalo ambalo linachangia kupotea kwa haki za watoto hao.
Mkutano huo wa siku tatu unaendelea kufanyika mazizini imekusudia kufanya tathmini ya mwaka katika sekta ya elimu ili kujua namna ya kupunguza matatizo yanayoikabilia sekta hiyo.
Chanzo cha Habari:
http://zanzibar24.co.tz/2018/02/19/wizara-ya-elimu-imewataka-walimu-nchini-watakiwa-kujiendeleza-kitaaluma/
Comparte este contenido: